KINDA AJITABILIA MAZURI
Na Eligius
Nyoni
MCHEZAJI kinda wa klabu ya majimaji ya mkoani
Ruvuma, Antony Mwingira amesema kwamba licha ya yeye kuwa ndio mara yake ya kwanza kucheza
katika ligi kuu ya Tanzainia ameaidi kufanya mazuri kama atapewa nafasi ya
kucheza katika kikosi hicho.
Mwingira ambaye amekuwa mchango mkubwa katika timu
hiyo na kuisababisha kupanda daraja na
kuweza kurudi katika ligi kuu ya Tanzania inayofahamika kama VPL.
Mwingira ambaye kabla ya kujiunga na majimaji
alikuwa akizichezea timu za madaraja tofauti ili kuweza kuimarisha kiwango
chake kisi potee na klabu ambazo amezichezea
ni Miembeni Fc, Stand Fc, na Magima Fc iliyopo Peramiho mkoani Ruvuma.
Akizungumza na Taifa Letu, Mwingira alisema kwamba
yeye ni mchezaji na yuko tayari kwa michezo ya ligi kuu kama atapewa nafasi ya
kucheza mara kwa mara katika timu.
Mchezaji huyo anbaye anapenda kuvaa jezi namba 16,
na hakusita kusema mchezaji ambaye anavutiwa nae hapa nchini ni, Simon Msuva na kule ulaya
anampenda Christian Rolnado.
“Mimi ni mwanajeshi, nitakwenda vitani kupambana ili
kuakikisha timu yangu ya majimaji inashinda kila mechi ambayo nitacheza,.”
Alisema kwamba kila mchezaji ana nafasi ya kucheza
katika timu, na ushirikiano kati yake na wachezaji wenzake wote wanaushirikiano mzuri na wako tayari
kupambana.
“Ili kuwa mchezaji bora lazima kufuata yale
tunayofundishwa na mwalimu ili tuweze kufanya vizuri katika michezo yetu
itakayoanza kutimua vumbi tarehe
12 septemba ambayo majimaji tutafungua daluga letu na Jkt Ruvu katika uwanja
wetu wa majimaji hapa mkoani Ruvuma,.”Aliongeza mwingira
Comments
Post a Comment