Posts

Showing posts from February, 2015

Mtoto mkubwa azaliwa Marekani

Image
                                   Avery mtoto mkubwa kuliko kawaida nchini Marekani  Mwanamke mmoja nchini Marekani amejifungua mtoto mwenye uzito wa paundi 14.1 sawa na kilo 6.4kg na sasa mtoto huyo anakula mara mbili zaidi ya uwezo wa mtoto mchanga . BiMaxxzandra Ford amepata mtoto aliyempa jina Avery, ndiye mtoto mkubwa na mzito kuwahi kuzaliwa katika hospitali ya wanawake ya mtakatifu Joseph iliyoko Tampa, Florida.Avery, alizaliwa kwa njia ya kawaida . Ford alikuwa hajatanabahi kuwa yu mjamzito mpaka alipotimiza wiki 35 .lakini mara baada ya kuwa anaongezeka uzito kupita kiasi ,madaktari wakamthibitishia kuwa yu mja mzito,na kutokana na kasi ya unenepaji mwanzo Bi Ford alihisi atajifungua watoto pacha,kumbe sivyo. Debbie Moore, mkunga katika hospitali hiyo, wasingemru...

Wapinzani walalamikia uchaguzi Nigeria

Image
                                                                 Muhammadu Buhari Upinzani nchini Nigeria umekosoa hatua ya kuahirishwa kwa uchaguzi hadi mwishoni mwa Mwezi March. Chama kikuu cha upinzani cha APC kimesema hatua hiyo ni kikwazo kikubwa kwa Demokrasia nchini humo. Chama hicho kimedai kuwa Jeshi la Nigeria limelazimisha kuahirishwa kwa Uchaguzi ili liweze kumsaidia Rais wa nchi hiyo, Goodluck Jonathan kwenye Kampeni zake. Uchaguzi mkuu nchini humo ulipangwa kufanyika jumamosi ijayo lakini Tume ya Uchaguzi imesema Mashambulizi ya Boko Haram kwa kiasi kikubwa yanahatarisha uwepo wa zoezi la uchaguzi ,Usalama wa Wapigakura, na wa...

Alichokijibu Mbunge Mbatia kuhusu ishu ya kusema kuwa Mrema ni mgonjwa.

Image
Mbunge wa Vunjo, Augustine Mrema (TLP) alitoa hoja binafsi Bungeni kwamba Mbunge James Mbatia amekuwa akipita Jimbo la Vunjo na kuwaambia wapigakura wasimchague Mrema kwa sababu ni mgonjwa. “ Napenda kusema kuwa mimi ni mbunge halali wa Vunjo na Mbatia hatapata jimbo hilo na ninatangaza kuwa nitagombea tena na hafi mtu hapa “– Alisema  Mrema wakati akimalizia kuwasilisha hoja yake hiyo. Leo wakati wa kikao cha Bunge jioni, Mbunge Mbatia alipata nafasi kujibu kuhusu ishu hiyo; “ Maelezo haya nayatoa kukanusha kwa moyo wangu wote matamshi yaliyotolewa ndani ya Bunge hili na Mheshimiwa Augustine Lyatonga Mrema , Mbunge wa Vunjo. Siku ya tarehe 05/02/2015 wakati wa kuahirisha Bunge Mheshimiwa Mrema alitoa maelezo ambayo sio sahihi alipoeleza kuwa mimi James Francis Mbatia niliwahi kusema kuwa yeye ni mgonjwa anayeugua maradhi ya ukosefu wa kinga mwilini yaani UKIMWI“ “ Maelezo yote aliyoyatoa sio sahihi na sijawahi na sitawahi kutamka maneno hayo…  Sij...