SHAMBULIZI LAFANYIKA PWANI YA KENYA





Mashambulizi katika eneo la Mpeketoni kenya

Kuna Ripoti ya mashambulizi matatu katika maeneo ya pwani ya kenya karibu na mpaka wa kenya na Somali. 

Maafisa wa polisi wilayani Lamu wanachunguza milio mikali ya risasi iliosikika katika kituo kimoja cha kibiashara karibu na mji wa Mpeketoni ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa katika mashambulizi mawili mwezi uliopita.

Kusini mwa Mpeketoni, kituo kimoja cha polisi katika wilaya ya Tanaraiver kinadaiwa kushambuliwa huku baadhi ya nyumba zikichomwa.

Kundi la wapiganaji wa kisomali Al-shabaab limekiri kutekeleza shambulizi hilo bila ya kutoa maelezo zaidi.

Mwandishi wa BBC nchini kenya amesema kuwa kuna polisi wengi katika maeneo ya pwani kufuatia shambulizi hilo la mwezi uliopita.

Comments

Popular posts from this blog

Unajua kiungo kikubwa zaidi kwenye Mwili?, Unajua kina uzito gani? Fahamu hapa

MAMBO YA YANGA NA AL AHLY