SHAMBULIZI LAFANYIKA PWANI YA KENYA
Mashambulizi katika eneo la
Mpeketoni kenya
Kuna Ripoti ya mashambulizi matatu katika maeneo ya pwani ya kenya karibu na mpaka wa kenya na Somali.
Maafisa wa polisi wilayani Lamu
wanachunguza milio mikali ya risasi iliosikika katika kituo kimoja cha
kibiashara karibu na mji wa Mpeketoni ambapo zaidi ya watu sitini waliuawa
katika mashambulizi mawili mwezi uliopita.
Kusini mwa Mpeketoni, kituo kimoja
cha polisi katika wilaya ya Tanaraiver kinadaiwa kushambuliwa huku baadhi ya
nyumba zikichomwa.
Kundi la wapiganaji wa kisomali
Al-shabaab limekiri kutekeleza shambulizi hilo bila ya kutoa maelezo zaidi.
Mwandishi wa BBC nchini kenya
amesema kuwa kuna polisi wengi katika maeneo ya pwani kufuatia shambulizi hilo
la mwezi uliopita.
Comments
Post a Comment