Shughuli ya kupiga kura yaanza Afrika Kusini


Shughuli ya kupiga Nchini Afrika Kusini ilianza vyema mapema leo asubuhi huku idadi kubwa ya wapigaji kura ikijitokeza.

Zaidi ya watu million 25 nchini humo wanaendelea katika vituo vya upigaji kura kwa uchaguzi mkuu wa mara ya tano tangu kumalizika kwa utawala wa mtu mweupe.

Taarifa zinazohusiana na
Chama tawala cha African National Congress, ANC ndicho kilicho maarufu zaidi. Lakini umaarufu wa chama hicho na rais Jacob Zuma umeathirika kutokana na tuhuma za rushwa na matatizo ya kijamii.
Licha ya kukumbwa na kashfa za ufisadi na utawala mbovu, duru zinasema kuwa chama cha ANC huenda kikanyakuwa ushindi.
Uchaguzi huo unasimamiwa na maafisa zaidi ya 200,000 wa tume ya uchaguzi watakao zunguka mikoa yote 9 iliyoko nchini.


Comments

Popular posts from this blog

Unajua kiungo kikubwa zaidi kwenye Mwili?, Unajua kina uzito gani? Fahamu hapa

MAMBO YA YANGA NA AL AHLY