TFF YAJIPANGA KUKUZA WATOTO KWENYE MICHEZO
Rais wa shirikisho la mpira Nchini Tanzania TFF,JAMAL MALINZI amesema
kuwa anampango wa kukuza vipaji kwa vijana wa Tanzania ili kuweza kupata timu
ya Taifa iliyo kamilika ilikuweza kufika mafanikio na malengo ya kutaka kucheza
kombe la dunia mwaka 2018 ameyasema hayo alipotembelea shule za kukuza vipaji
jijini mwanza akiambatana na viongozi wenzie katika msafara huo.
Amesema kuwa lengo ni kufika mbali kisoka katika
nchi ya Tanzania “Nina mpango wa kuleta maendeleo katika ya kimpira katika nchi
ya Tanzania sababu ni kuweka mikakati ili kuweza kufanikiwa katika viwango vya
juu kisoka ili kuleta mabadiliko katika nchi yetu”
Pamoja na kusema hayo rais wa TFF pia akasema kuwa
ni lazima tupiganie kuweza kufika mafanikio ya kimpira katika nchi yetu na kusema
kuwa atakuwa mstari wa mbele akishirikiana na viongozi wenzake ili kuwezesha
kupata timu za Taifa zote kwa upande wa wavulava na wasichana .
Rais wa shirikisho ameendelea kusema kuwa”lakini
lazima kuwa na mikakati na mlengo muhimu ili kuweza kufika mbali kisoka kwa
sababu ukiwa malengo ni lazima ufanye kwa ubunifu zaidi ili kupata vitu vizuri
kwe mpira na ni wakati wa kubadilika kimawazo maana viongozi waliopita katika
shirikisho hili la mpira walikuwa wa maneno na sio vitendo zaidi”.
Hatimaye tutaweza kubadilika kwa sababu tumejipanga
vizuri katika swala la kukuza vipaji katika nchi yetu ili nasi tujivunie
mafanikio katika soka la Tanzania kwa kujitangaza kimataifa na tukifikia katika
malengo hayo nasi tutakuwa tunaweza kushindana katika mashindano ya ndani ya
nchi yetu na yale nje ya nchi.
Pamoja na hayo yote na serikali iko pamoja nasi
kuakikisha kuwa tunafika malengo ya kufanikiwa
na kuweza kujimudu wenyewe ili kuendeleza swala la mpira katika nchi
yetu ya Tanzania.
Comments
Post a Comment