Macho na masikio kwenu Azam na Yanga.


Vilabu viwili vya Tanzania bara Azam fc na Yanga ndivyo zilizopata jukumu la kushirik katika michuano ya Klabu bingwa Afrika.
 
Ushiriki wa vilabu hivyo umekuja baada ya vilabu hivyo kufanya vizuri katika michezo yao ya mwanzo ambazo Yanga ilishinda mabao 7-0 ilipokutana na wacomoro kutoka katika visiwa vya Comoro.

Azam nayo ilishinda kwa bao 1-0 pale ilipochuana vikali na Klabu moja kutoka Msumbiji.

Matokeo hayo yameziwezesha timu hazo kuiwakilisha Tanzania katika kushiriki michuano hiyo inayotarajiwa kufanyika Jumamosi hii ambapo Yanga itamenyana kwa mara ya pili na Wacomoro hao katika visiwa hivyo.

Azam nao wanatarajiwa kushuka dimbani siku ya jumapili hiihuko Msumbiji dhidi ya wanamsumbiji kwa mechi ya marudiano wakitafuta kucheza 16 bora ili waweze kuendelea na michuano hiyo.

Macho na masikio ya watanzania ni kwa timu hizo mbili kurudi na ushindi ili waweze kuingia katika michuano hiyo ya timu 16 bora.  

Comments

Popular posts from this blog

Unajua kiungo kikubwa zaidi kwenye Mwili?, Unajua kina uzito gani? Fahamu hapa

MAMBO YA YANGA NA AL AHLY